Na
Princess Asia
MICHUANO ya Airtel Rising Star, inayohusisha vijana
walio na umri chini ya miaka 17, inaanza leo mjini Najirobi, Kenya na itakuwa
ikirushwa live na Super Sport 9.
Kikosi cha wachezaji 16
watakaoiwakilisha Tanzania kwenye mashindano hayo
ya
kimataifa itakayofikia tamati
Agosti 25, mwaka huu tayari kipo
Nairobi kupeperusha bendera nzuri yenye za kijani, bluu, nyeusi na njano.
Kikosi hicho kinaundwa
na Denis
Richard, Juma Hamza, Abdul Selemani, Ishaka Shekolowa, Bakari Ally, Abdulatif Mohamed,
George Joseph, Badilu Said, Said
Kassim, Amos Ikungula, Paul Balama,
Goodluck
Mabiku, Joel Kasimula, Ibrahim Mtenga,
Sntkony Angelo na Suleiman Yunus.
Mashindano hayo yanayotarajiwa kuwa na ushindani mkali yatashirikisha
wachezaji wengine nyota wa ARS kutoka nchi za Kenya, Uganda, Malawi, DRC, Congo
Brazzaville, Nigeria, Ghana, Zambia, Niger, Gabon, Burkina Fasso, Sierra Leone,
Chad, Madagascar mbali na Tanzania.
Michuano hiyo itafuatiwa na kliniki ya soka ya kimataifa ambayo pia
itafanyika Nairobi chini ya walimu wa soka la vijana kutoka klabu maarufu
duniani ya Manchester United ya England. Kliniki kama hii
ilifanyika mwaka jana kwenye uwanja wa kisasa wa soka mjini Dar es Salaam na kushirikisha vijana kutoka Kenya, Malawi, Sierra
Leone na wenyeji Tanzania.
Katika kliniki ya mwaka huu, Tanzania itawakilishwa na wachezaji sita
miongoni mwao ni wavulana watatu na wasichana watatu ambao walioibuka kuwa
wachezaji bora wakati wa fainali za Taifa jijini Dar es Salaam mwezi Juni.
Airtel Rising Stars ni mpango kabambe wa kuibua na kukuza vipaji vya
wanasoka wanaochipukia barani Afrika. Walengwa ni wavulana na wasichana wenye
umri chini ya miaka kumi na saba ambao watapata fursa ya pekee ya kuonyesha
vipaji vyao mbele ya waatalum wa mpira wa miguu wa kitaifa na kimataifa.



.png)
0 comments:
Post a Comment