MAZISHI ya mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki dunia jana asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam.
Mwimbaji huyo aliyetesa kwa sauti yake tamu na kwa tungo zake za kusisimua, amezikwa katika makaburi ya Kisutu huku idadi kubwa ya wanamuziki wa fani mbalimbali ikiwa sehemu ya umati uliofurika makaburini hapo.
Aidha, Dede pia amezikwa na vigogo wengi wa dini ya Kiislam, maofisa wengi wa serekali na wanamichezo maarufu.
Watu wakiwa wamebeba jeneza la mpendwa wao, Shaaban Dede Adhuhuri ya leo kwenda kumpumzisha katika nyumba yake ya milele PICHA ZAIDI GONGA HAPA
Pengine kwa miaka ya hivi karibuni, ukiondoka msiba wa marehemu Muhudini Gurumo, hakuna tena msiba wa mwanamuziki wa dansi uliohudhuriwa na watu wengi kama huu wa Dede.
Mwimbaji huyo aliyetesa kwa sauti yake tamu na kwa tungo zake za kusisimua, amezikwa katika makaburi ya Kisutu huku idadi kubwa ya wanamuziki wa fani mbalimbali ikiwa sehemu ya umati uliofurika makaburini hapo.
Aidha, Dede pia amezikwa na vigogo wengi wa dini ya Kiislam, maofisa wengi wa serekali na wanamichezo maarufu.
Watu wakiwa wamebeba jeneza la mpendwa wao, Shaaban Dede Adhuhuri ya leo kwenda kumpumzisha katika nyumba yake ya milele PICHA ZAIDI GONGA HAPA
Pengine kwa miaka ya hivi karibuni, ukiondoka msiba wa marehemu Muhudini Gurumo, hakuna tena msiba wa mwanamuziki wa dansi uliohudhuriwa na watu wengi kama huu wa Dede.
0 comments:
Post a Comment