• HABARI MPYA

    Tuesday, July 11, 2017

    JAMES RODRIGUEZ ATUA KWA MKOPO MIAKA MIWILI BAYERN MUNICH

    KIUNGO mshambuliaji wa Real Madrid, James Rodriguez amesaini mkataba wa miaka miwili kujiunga na Bayern Munich kwa mkopo ambako anakwenda kuungana na kocha wake wa zamani, Mtaliano Carlo Ancelotti.
    Rodriguez atafanyiwa vipimo vya afya na vigogo hao wa Ujerumani kabla ya kukamilisha uhamisho wake kwenda Allianz Arena - katika dili ambalo litagharimu hadi Pauni Milioni 40.
    Bayern pia itakuwa na nafasi ya kumnunua moja kwa moja mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Colombia mwishoni mwa mkopo huo Juni 30, mwaka 2019.


    Kiungo mshambuliaji wa Real Madrid, James Rodriguez amesaini mkataba wa miaka miwili kujiunga na Bayern Munich PICHA ZAIDI GONGA HAPA 

    Mkataba wa sasa wa mkopo unagharimu Pauni Milioni 9 na Pauni Milioni 31 nyingine zitaongezwa iwapo mwishowe watataka kumnunua moja kwa moja mchezaji huyo.
    Atakuwemo kwenye kikosi cha Bayern ambacho Jumapili jioni kitakwenda kwenye michuano ya siku 12 ya Audi Summer Tour nchi za China na Singapore.
    Mwenyekiti wa Bayern, Karl-Heinz Rummenigge ameelezea furaha yake baada ya kumpata mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 akisema kwamba alikuwa chaguo kuu la Ancelotti katika dirisha hili. 
    Ancelotti na Rodriguez walifanya kazi pamoja Real Madrid baada ya mchezaji huyo kujiunga na timu hiyo kwa dau la Pauni Milioni 63 mwaka 2014.
    Katika msimu wao mmoja wa kufanya kazi pamoja Jiji Kuu la Hispania, walishinda mataji mawili ya UEFA Super Cup na Klabu Bingwa ya Dunia ya FIFA.
    Pamoja na hayo, kufuatia kufukuzwa kwa Ancelotti mwaka 2015 - umuhimu wa Rodriguez ukaanza kupungua Uwanja wa Santiago Bernabeu.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: JAMES RODRIGUEZ ATUA KWA MKOPO MIAKA MIWILI BAYERN MUNICH Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top