|
MSHAMBULIAJI nyota wa Burkina Faso, Jonathan Pitroipa, ambaye alilimwa kadi nyekundu katika Nusu Fainali Jumatano anajiandaa kucheza Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika Jumapili dhidi ya Nigeria.
Hadi Pitroipa kuwa tayari kucheza mechi ya Jumapili, ilibidi refa wa Jumatano kati ya Burkina Faso na Ghana, Slim Jdidi wa Tunisia akiri alifanya makosa kumpa kadi ya pili ya njano mchezaji huyo kwa kujirusha, amesema rais wa CAF, Issa Hayatou.
"Kila mtu anasema huyu refa hakuchezesha vizuri hii mechi," alisema Hayatou leo.