• HABARI MPYA

    Monday, August 14, 2017

    RONALDO AFUNGIWA MECHI TANO KWA KUMSUKUMA REFA JANA

    MWANASOKA bora wa dunia, Cristiano Ronaldo amefungiea mechi tano na kupigwa faini ya Pauni 2,700 kwa kumsukuma refa, Ricardo de Burgos Bergoetxea baada ya kuonyeshwa kadi ya pili ya njano.
    Ronaldo alitolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 82 baada ya kuonyeshwa kadi ya pili ya njano jana katika mchezo wa kwanza wa Super Cup ya Hispania Uwanja wa Camp Nou, Real Madrid ikishinda 3-1 dhidi ya wenyeji, Barcelona.
    Mreno huyo alionyeshwa kadi ya kwanza ya njano dakika moja iliyotangulia baada ya kuvua jezi wakati wa kushangilia bao la pili la timu yake alilofunga dakika ya 80 kabla ya kuonyeshwa kadi ya pili kwa kujiangusha kufuatia kukutana na Samuel Umtiti.
    Kifungu cha 96 cha kanuni kinasema kwamba mchezaji anayemvaa refa kwa kumvuta, kumsukuma au kumtikisa atahesabika amefanya kosa la kumfanyia vurugu mwamuzi na adhabu yake ni kufungiwa kati ya mechi nne hadi 12.


    Cristiano Ronaldo akimsukuma refa Ricardo De Burgos Bengoetxea baada ya kuonyeshwa kadi ya pili ya njano na kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 82 jana 
    PICHA ZAIDI GONGA HAPA  
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RONALDO AFUNGIWA MECHI TANO KWA KUMSUKUMA REFA JANA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top