TIMU ya Simba SC imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji, Mtibwa Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Mabao ya Simba SC yamefungwa na beki Rushine De Reuck kutoka Afrika Kusini kwa penalti dakika ya tisa, mshambuliaji mzawa, Suleiman Abdallah Mwalimu dakika ya 77 na winga Muivory Coast, Alain Anicet Oura dakika ya 90
Kwa ushindi huo, Simba SC inafikisha pointi 67, ingawa inabaki nafasi ya pili ikizidiwa pointi mbili na mabingwa watetezi, Yanga SC – wakati Mtibwa Sugar inabaki na pointi zake 27 na kushukia nafasi ya 14 kwenye ligi ya timu 16 kufuatia timu zote kucheza mechi 28.
Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja moja kwa moja na nyingine mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu.
Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndiye atacheza Ligi Kuu msimu ujao.



.png)
0 comments:
Post a Comment