// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); TAIFA STARS YAPANGWA NA DRC, GUINEA NA ETHIOPIA KUWANIA TIKETI YA AFCON 2025 - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE TAIFA STARS YAPANGWA NA DRC, GUINEA NA ETHIOPIA KUWANIA TIKETI YA AFCON 2025 - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Thursday, July 04, 2024

    TAIFA STARS YAPANGWA NA DRC, GUINEA NA ETHIOPIA KUWANIA TIKETI YA AFCON 2025

    TANZANIA imepangwa Kundi H pamoja na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Guinea na Ethiopia kuwania tiketi ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika nchini Morocco mwaka 2025.
    Katika Droo iliyopangwa leo Jijini Johannesburg, Afrika Kusini, mabingwa watetezi, Ivory Coast wamepangwa Kundi G pamoja na Zambia, Sierra Leone na Chad.
    Jumla ya nchi 52 zinatarajiwa kushiriki hatua ya makundi ya kuwania tiketi ya AFCON 2025 kuanzia Septemba 2 hadi Novemba 19 mwaka huu na washindi wawili wa makundi yote 12 watatengeneza idadi ya timu 24 wakiwemo wenyeji Morocco, kufuzu AFCON ya mwakani.

    MAKUNDI YOTE KUFUZU AFCON 2025 MOROCCO
    Kundi A: Tunisia, Madagascar, Comoros, Gambia
    Kundi B: Morocco, Gabon,Central Africa Republic, Lesotho 
    Kundi C: Egypt, Cape Verde, Mauritania, Botswana
    Kundi D: Nigeria, Benin Libya, Rwanda 
    Kundi E: Algeria, Equatorial Guinea, Togo, Liberia
    Kundi F: Ghana, Angola, Sudan, Niger
    Kundi G: Cote d'Ivoire, Zambia, Sierra Leone, Chad
    Kundi H: DR Congo, Guinea, Tanzania, Ethiopia
    Kundi I: Mali, Mozambique, Guinea Bissau, Eswatini
    Kundi J: Cameroon, Namibia, Kenya, Zimbabwe
    Kundi K: South Africa, Uganda, Congo, South Sudan
    Kundi L: Senegal, Burkina Faso, Malawi, Burundi


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TAIFA STARS YAPANGWA NA DRC, GUINEA NA ETHIOPIA KUWANIA TIKETI YA AFCON 2025 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top