Robin Gibb amefariki akiwa ana miaka 62
MWIMBAJI wa kundi la Bee Gees, Robin Gibb, amefariki dunia jana akiwa ana umri wa miaka 62.
Mwimbaji huyo ambaye ameuza nakala zaidi ya Milioni 200 na kutoa nyimbo kibao zilizotikisa akiwa na ndugu zake Maurice na Barry, alifanyiwa upasuaji na akakutwa na maradhi ya saratani.
Familia ya Robin Gibb wa kundi lililokuwa likiundwa na ndugu, Bee Gees imetangaza kwa machungu makubwa kifo cha Robin leo.
Robin Hugh Gibb alizaliwa Desemba 22, mwaka 1949 kabla ya kifo chake jana Mei 20, 2012 na alikuwa mweanamuziki maarufu Uingereza na mtunzi pia. Umaarufu wake ulitokana na kundi la Bee Gees, alilokuwa akipiga kazi na ndugu zake, pacha wake Maurice na kaka yake Barry. Mdogo wake mwingine, Andy Gibb, pia ni mwanamuziki maarufu wa kujitegemea.
Robin Hugh Gibb alizaliwa Desemba 22, mwaka 1949 kabla ya kifo chake jana Mei 20, 2012 na alikuwa mweanamuziki maarufu Uingereza na mtunzi pia. Umaarufu wake ulitokana na kundi la Bee Gees, alilokuwa akipiga kazi na ndugu zake, pacha wake Maurice na kaka yake Barry. Mdogo wake mwingine, Andy Gibb, pia ni mwanamuziki maarufu wa kujitegemea.
Mara ya mwisho, Gibb alionekana jukwaani akitumbuiza Februari mwaka huu katika shoo ua hisanihuko London Palladium.
Robin na kundi lake Bee Gees na kaka zake Maurice, aliyefariki dunia mwaka 2003 na Barry ambaye sasa ni pekee aliyebaki.
Robin Gibb jukwani na ndugu zake Maurice (kushoto) na Barry (kulia) katika tamasha la Bee Gees mjini Sydney mwaka 1999
Mwaka 2004 Robin na kaka yake, Barry
1970
Robin Gibb 1978
Robin 1991 |
Robin 1981
1983: Robin Gibb na mkewe Dwina na mtoto wao wa kiume, Robin-John, anayefahamika kama RJ
0 comments:
Post a Comment