Football | Barclays Premier League
| |
|
KOCHA wa Newcastle, Alan Pardew ameshinda
tuzo ya kocha bora wa Ligi Kuu ya England, baada ya kufanya mambo makubwa akiwa
na Magpies akiiwezesha kuwania kumaliza ndani ya Top-Four.
Newcastle ilitarajiwa kusota msimu huu,
baada ya kuondoka kwa Kevin Nolan na Joey Barton, ambao walimfuatia mshambuliaji
Andy Carroll aliyeondoka Januari mwaka jana kujiunga na Liverpool.
Pamoja na hayo, kuteuliwa katika mazingira
ya utata kwa Pardew kuchukua nafasi ya Chris Hughton Desemba mwaka 2010, kumeisaidia
Newcastle kuzinduka na kufanya mavitu, kiasi kwamba bado wamo kwenye kinyang’anyiro
cha kucheza Ligi ya Mabingwa msimu ujao, hatima yao ikiwa itajulikana katika
mechi za mwisho Jumapili.
.
0 comments:
Post a Comment