• HABARI MPYA

    Monday, June 24, 2019

    ARGENTINA YAIPIGA QATAR 2-0, YATINGA ROBO FAINALI COPA AMERICA

    Sergio Aguero akishangilia baada ya kuifungia bao la pili Argentina dakika ya 82 katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Qatar na kuihakikishia kutinga Robo Fainali ya michuano ya Copa America usiku wa jana Uwanja wa Arena do Gremio mjini Porto Alegre, Rio Grande do Sul na itamenyana na Venezuela Juni 28. Bao la kwanza limefungwa na Lautaro Martinez dakika ya nne na kwa matokeo hayo inamaliza nafasi ya pili kwenye Kundi B kwa pointi zake nne, nyuma ya Colombia iliyoongoza kwa pointi tisa, Paraguay imemaliza nafasi ya tatu kwa pointi zake mbili na Qatar iliyoambulia pointi moja imeshika mkia 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ARGENTINA YAIPIGA QATAR 2-0, YATINGA ROBO FAINALI COPA AMERICA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top