• HABARI MPYA

    Sunday, June 16, 2019

    AZAM FC NA MTIBWA SUGAR ZATINGA NUSU FAINALI YA LIGI KUU YA VIJANA U20

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    TIMU ya vijana ya Azam FC (Azam U-20) imetinga nusu fainali ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwa vijana chini ya umri wa miaka 20 (U-20 Premier League) baada ya kuichapa Biashara United mabao 3-1 usiku huu.
    Huo ni ushindi wa pili mfululizo kwa kikosi hicho kwenye hatua ya nane bora ya michuano hiyo ikiwa Kundi B, ambapo mechi ya kwanza iliichapa Tanzania Prisons 2-0.
    Mabao ya Azam U-20 usiku huu yamefungwa na nahodha wa timu hiyo, Lusajo Mwaikenda, Abadi Kawambwa na Agiri Ngoda, aliyehitimisha ushindi huo.

    Mbali na Azam U-20, timu nyingine ya kundi hilo iliyofuzu nusu fainali ni Mtibwa Sugar, iliyoichapa Prisons 3-1 kwenye mchezo wa awali uliofanyika jioni.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC NA MTIBWA SUGAR ZATINGA NUSU FAINALI YA LIGI KUU YA VIJANA U20 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top