BONDIA Floyd Mayweather amemzidi nusu kilo Marcos Maidana wakati wa kupima uzito kuelekea pambano la usiku wa leo mjini Las Vegas.
Mkali huyo wa kutupa mikono kwa kasi pia anapungua nusu kilo kutimia uzito kamili wa paundi 147 wa mataji ya Welter na Light Middle.
Mayweather atapambana na mbabe wa Argentina ukumbi wa MGM Grand Garden Arena usiku wa leo, katika pambano la marudiano baada ya Mei kushinda kwa utata.
Nakudunda tena; Floyd Mayweather na Marcos Maidana wakitazamana wakati wa kupima uzito mjini Las Vegas katika ukumbi wa MGM Grand
Safari hii nakupiga; Floyd Mayweather na Marcos Maidana wakiwa wameshikilia mkanda wa WBC wakati wa kupima uzito MGM Grand Garden Arena
Floyd Mayweather wakati akipima uzito Las Vegas leo
Marcos Maidana wakatiakipima uzito



.png)
0 comments:
Post a Comment