• HABARI MPYA

    Saturday, September 27, 2014

    MESSI AFIKISHA MABAO 401 BARCA IKIUA 6-0 LA LIGA, NEYMAR APIGA HAT TRICK YA KWANZA CAMP NOU

    MSHAMBULIAJI Leonel Messi amefikisha mabao 401 leo Barcelona ikishinda 6-0 dhidi ya Granada katika La Liga usiku huu Uwanja Camp Nou.
    Lakini shujaa wa mchezo alikuwa Mbrazil, Neymar aliyefunga mabao matatu peke yake, hiyo ikiwa hat trick yake ya kwanza tangu ametua Camp Nou.
    Messi kwa kufunga mara mbili leo, sasa ana mabao 401 aliyoifungia Barca na nchi yake, Argentina katika mechi 524 jumla alizocheza akiwa ana umri wa miaka 27 tu. Bao lingine la Barca limefungwa na beki Ivan Rakitic.
    Ushindi huo unakuja wakati kikosi cha Luis Enrique kinaelekea kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Jumanne mjini Paris dhidi ya PSG.
    Neymar na Messi wakipongezana kwa kazi nzuri leo
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MESSI AFIKISHA MABAO 401 BARCA IKIUA 6-0 LA LIGA, NEYMAR APIGA HAT TRICK YA KWANZA CAMP NOU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top