• HABARI MPYA

    Wednesday, September 24, 2014

    RONALDO SI WA KAWAIDA, HIZO REKODI ANAZOVUNJA NI BALAA!

    • MWANASOKA bora wa dunia, Cristiano Ronaldo amezidi kuweka rekodi ngumu katika ulimwengu wa soka, baada ya jana kufunga mabao manne katika ushindi wa 5-1 dhidi ya Elche katika La Liga.
      Katika mabao hayo manne, mawili yalikuwa ya penalti na hiyo inamaanisha Ronaldo anawea kufunga kila wakati Real Madrid ikizawadiwa tuta. 
      Unaweza kutundika matairi kadhaa ya gari pembezoni mwa lango na umuambie bao litahesabiwa pale tu atakpopitisha mpira katikati yake mojawapo, na kisha uweke makipa wawili kwenye mstari, na bado atafunga.
      "Si kawaida" hivyo ndivyo makocha wengi wa timu pinzani wamekuwa wakisema kuhusu yeye tangu aibuke mfungaji bora wa jumla wa Real Madrid miaka mitano iliyopita. Na hapana, si kawaida,".

      RONALDO THE RECORD-BREAKER 

      Zifuatazo ni baadhi ya rekodi ambazo Cristiano Ronaldo anazoshikilia:
      • Mabao mengi aliyofunga msimu mmoja kwenye Kombe la Ulaya: 17
      • Mchezaji pekee kushinea kiatu cha dhahabu Ulaya katika ligi mbili tofauti (Ligi Kuu England akiwa na Manchester United na La Liga akiwa na Real Madrid)
      • Mchezaji wa kwanza kufunga dhidi ya timu kila timu katika msimu mmoja La Liga 
      • Mabao mengi aliyofunga kwenye mashinano yote Real Madrid kwa msimu: 60
      • Hat-trick nyingi alizofunga kwa msimu mmoja Real Madrid: 7
      • Mchezaji aliyefunga mabao 250 kwa haraka zaidi Real Madrid 
      • Mfungaji bora wa kihistoria Ureni kwa mabao yake 50

        MABAO YA RONALDO KWA UJUMLA 

        Mwaka           Timuu                      Mechi  Mabao 
        2002-2003     Sporting Lisbon       31      5
        2003-2009     Manchester United  292    118
        2009-             Real Madrid             254    264
        2003-             Ureno                       114    50

      REKODI ZAIDI ZA RONALDO ZINAKUJA... 

      • Mabao tisa aliyofunga Ronaldo katika mechi tano za La Liga ni moja zaidi ya Lionel Messi wakati nyota huyo wa Barcelona alipofikisha mabao 50 katika La Liga msimu wa 2011-12
      • Akiwa na mabao 264 katika miaka yake mitano ya kucheza Real Madrid, Ronaldo anahitaji manbao 59 kumfikia Raul aliyefunga mabao 323, kwa zaidi ya miaka 16.
      • Ronaldo sasa amefikisha hat trick 21 katika La Liga, mbili zaidi ya Messi na moja nyuma ya anayesukilia rekodi, Alfredo Di Stefano
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RONALDO SI WA KAWAIDA, HIZO REKODI ANAZOVUNJA NI BALAA! Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top