Kocha wa twiga, Charles Boniface Mkwasa akishuhudia mvua ya mabao |
TIMU ya taifa ya soka ya wanawake ya
Tanzania, Twiga Stars kwa ‘bakhti mbaya’ leo imechapwa mabao 4-1 katika mchezo
wa kimataifa wa kirafiki uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mchezo huo ulikuwa ni hamususi kwa kuzinoa
timu hizo zinazojiwinda na mechi zake za kuwania kucheza fainali za Afrika kwa
Wanawake (AWC) ambazo Twiga itakwaana na Etthiopia Mei 26 mwaha huu huku
Zimbabwe itakipiga na Nigeria.
Kipigo cha Twiga dhidi ya Zimbabwe ni mara ya pili ambapo mara ya kwanza ilikuwa nusu fainali ya
Kombe la COSAFA ambapo katika mechi hiyo iliyochezwa Julai 5 jijini Harare ,
Zimbabwe ilishinda kwa penalti 4-2.
Aidha, timu ambazo jana ilikuwa mara ya
tatu kukutana, mara ya pili walkikwaana kwenye michezo ya All Africa Games
(AAG) iliyofanyika Maputo , Msumbiji ambapo timu hizo zilitoka sare ya mabao
2-2.
Katika mchezo wa jana, Rufaro Machungura
aliiandikia Zimbabwe bao la kwanza katika dakika ya 5 ya mchezo baada ya mabeki
wa Twiga kujichanganya.
Dakika ya 17 Nokuthula Ndolovu alimalizika
kazi nzxuri ya washambuliai wake kwenye eneo la hatari na kuandika bao la la pili ambalo lilidumu
hadi timu hizo zinakwenda mapumziko ambapo Zimbabwe ilikuwa ikiongoza mabao
2-0.
Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote
kucheza kwa taratibu kabla ya Asha Rashid kuiandikia Twiga bao lake pekee
katika dakika ya 46 akimalizia kazi nzuri ya Mwanahamis Omari.
Zimbabwe ilitikisa nyavu za Twiga kwa mara
ya tatu katika dakika ya 54 kupitia kwa Nokuthula alipotumia vema uzembe wa
beki wa Twiga Fatma Khatib aliyerkuwa katika harakati za kuokoa krosi yake.
Rufaro Machungura alifunga karamu ya mabao
kwa Zimbabwe katika dakika ya 74 ambalo lililidumu hadi dakika 90 ya mchezo huo
iliyomalizika kwa Zimbambwe kushinda 4-1.
Aidha, mchezo huo ambao ulichelewa kupigwa
kutoka na mvua iliyonyesha jana jijini Dar es Salaam, Mwamuzi wa kimataifa
JudithhGamba alimzawadia kadi ya njano nyota wa Twiga Fatma Bashir kwa kumchezea vibaya Rufaro.
Katika mchezo huo Twiga ilifanya mabadiliko
na kuwatoa Rukia Khamis, , Zena Khamis , Mwajuma Abdallah,na Fatma Hatib na
kuwaingiza kuwaingiza Fadhila
Hamadi, Amina Ally, Siajab Hassan na
Mwanaid Tamba.
Baada ya mchezo huo Twiga ambayo ilipata
nafasi nyingi za wazi na kushindwa kuzitumia walidai kufungwa kwao kulichangiwa na mvua.
0 comments:
Post a Comment