AFRIKA Kusini leo imetaja miji mtano
itakayokuwa wenyeji wa Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwakani,
inayotarajiwa kuanza Januari 19 hadi Februari 10, 2013.
Majiji hayo matano ni Johannesburg katika Uwanja
wa Soccer City, Port Elizabeth katika Uwanja wa Nelson Mandela Bay, Rustenburg
katika Uwanja wa Royal Bafokeng, eThekwini katika Uwanja wa Moses Mabhida na
Mbombela katika Uwanja wa Mbombela.
Waziri wa Michezo wa Afrika Kusini, Fikile
Mbalula pia alisema sherehe za ufunguzi na kufunga michuano hiyo, zitafanyika
kwenye Uwanja wa Soccer City, Johannesburg.
Pia, ratiba ya michuano hiyo itapangwa
Oktoba 26, mwaka huu.
Afrika Kusini walikuwa wenyeji wa Fainali
za Mataifa ya Afrika mara moja tu mwaka 1996, walipoibuka mabingwwa na mwaka
juzi, waliweka rekodi ya kuwa nchi ya kwanza ya Afrika kuwa mwenyeji wa Fainali
za Kombe la Dunia
.
0 comments:
Post a Comment