• HABARI MPYA

    Thursday, September 04, 2014

    VAAN GAAL 'ATENGWA' MKUTANO WA MAKOCHA BABU KUBWA ULAYA MWENYEKITI GERGUSON

    KOCHA mpya wa Manchester United hakuwepo kwenye mkutamo wa makocha babu kubwa duniani wa kila mwaka, uliofanyika mjini Nyon, Usiwsi.
    Jana na leo, kocha wa zamani wa Manchester United, Sir Alex Ferguson amekuwa Mwenyekiti wa Mkutano wa 16 wa makocha duniani, ujulikanao kama Elite Club Coaches Forum kama balozi wa makocha wa UEFA ambao ulihudhuriwa pia na rais wa shirikisho hilo la soka Ulaya, Michel Platini.
    Ferguson alipigwa picha akitaniana na mpinzani wake wa zamani kazini Arsene Wenger wa Arsenal, wakati kocha wa Manchester City, Manuel Pellegrini alikuwepo pia.
    Picha ya timu:Mkutano wa Makocha uliofanyika makao makuu ya UEFA nchini Usiwsi (akiwemo Pep Guardiola na Luis Enrique)

    Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho amehudhuria mkutano huo pamoja na makocha wa zamani wa Stamford Bridge, Andre Villas-Boas, Rafael Bentiez na Carlo Ancelotti.
    Luis Enrique aliketi jirani na kocha wa zamani wa Barcelona, Pep Guardiola katika picha ya pamoja.
    All smiles: Sir Alex Ferguson chats with Carlo Ancelotti and Arsene Wenger at the managers' meeting in Nyon
    Sir Alex Ferguson akizungumza na Carlo Ancelotti na Arsene Wenger katika mkutano huo mjini Nyon 
    Discussions: Chelsea manager Jose Mourinho sits with former Stamford Bridge boss Ancelotti
    Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho na kocha wa zamani wa Stamford Bridge, Carlo Ancelotti
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: VAAN GAAL 'ATENGWA' MKUTANO WA MAKOCHA BABU KUBWA ULAYA MWENYEKITI GERGUSON Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top