TIMU ya soka ya taifa ya wanawake, Twiga
Stars itacheza na Zimbabwe katika mchezo wa kirafiki utakaofanyika Jumamosi wiki hii kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania
(TFF), Boniphace Wambura Mgoyo ameiambia BIN ZUBEIRY leo mchana kwamba
Twiga Stars hivi iko katika ziara ya mechi
za kirafiki katika mikoa ya Dodoma na Mwanza. Leo (Mei 8 mwaka huu) itacheza na
kombaini ya Mkoa wa Dodoma ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 katika mchezo
utakaofanyika Uwanja wa Jamhuri, mjini Dodoma.
Wambura amesema kesho (Mei 9 mwaka huu)
itaondoka kwenda jijini Mwanza ambapo pia itacheza mechi moja ya kirafiki Mei
10 mwaka huu kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, na kurejea Dar es Salaam tayari kwa
ajili ya mechi dhidi ya Zimbabwe.
Amesema Zimbabwe inatarajia kuwasili kesho
(Mei 9 mwaka huu) jioni kwa ndege ya South African Airways (SAA) ikiwa na
msafara wa 25 na wataondoka Mei 14 mwaka huu alfajiri.
0 comments:
Post a Comment