Mashabiki wa Simba waliokuwa wengi zaidi jana uwanjani |
KIASI cha Sh. Milioni 260 kimepatikana kutokana
na mechi ya funga dimba ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baina ya watani
wa jadi SImba na Yanga kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, kutokana na idadi
ya watu 41,733 walioingia.
Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania
(TFF), Boniphace Wambura Mgoyo, ameiambia BIN ZUBEIRY machana huu kwamba, watazamaji
4 viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya bluu na
kijani, sh. 10,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 20,000 VIP C, sh. 30,000 VIP
B na sh. 40,000 VIP A. Alisema watazamaji 36,980 walinunua tiketi za sh. 5,000
wakati 203 walikata za sh. 40,000 na jumla ya Sh. 260,910,000 zilipatikana.
Alisema Kila klabu ilipata Sh.
62,646,395.85, wakati asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ni Sh.
39,799,830.51 na TFF ilijimegea Sh. 19,908,361.95.
Alisema gharama za mechi kabla ya mgawo ni
nauli ya ndani ya waamuzi na kamishna sh. 20,000, posho ya kujikimu kwa
kamishna sh. 40,000 na mwamuzi wa akiba sh. 30,000, gharama za tiketi sh.
8,539,950, maandalizi ya uwanja (pitch preparation) sh. 400,000, umeme sh.
300,000, ulinzi na usafi wa uwanja sh. 2,350,000 na Wachina (Beijing
Construction) sh. 2,000,000.
Alisema mgawo wa uwanja ni sh.
19,908,361.95, gharama za mechi sh. 19,908,361.95, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira
wa Miguu (FDF) sh. 9,954,180.97, Baraza la Michezo la Taifa (BMT) sh.
1,990,836.19 na Chama cha Soka Dar es Salaam (DRFA) kilimegewa Sh.
10,467,324.78.
0 comments:
Post a Comment