Published: Today at 00:13
MWANASOKA nyota, Djibril Cisse anakabiliwa
na matatizo polisi baada ya shabiki kushambuliwa na genge la wahuni nje ya
jumba la sinema.
Mshambuliaji huyo wa QPR alizozana na
Geoffrey Candia, ambaye alimuomba kupiga naye picha wakiwa kwenye jumba la
sinema.
Wakati Geoffrey, 20 na wenzake watatu
walipoanza kupiga yowe kuita jina la nyota huyo, Cisse aliwataka kunyamaza
alimchukua mke wake kuona American Pie: Reunion.
Saa moja baadaye tangu sinema ianze, mtu
mmoja alisema Geoffrey ametoka Vue Cinema kwenda Park Royal, West London.
Alisema: “Nje alivamiwa na watu kama nane. Walikuwa wanamsubiri kwenye eneo la
magari.
“Walikuwa wakisema watavunja miguu yetu na
kutuulia mbali.”
Geoffrey alisema mmoja wa wahuni hao
alimpiga sana miguuni kabla hajaondoka.
Polisi kwanza inaangali rekodi ya tukio
hilo kewenye kamera za CCTV kabla ya kuamua kuzungumza na mwanasoka huyo wa
kimataifa wa Ufaransa mwenuye umri wa miaka 30.
Geoffrey, kutoka Harrow, North West London,
alipomuona mara ya kwanza baba wa watoto watatu, Cisse hakujwa na uhakika kama
ni yeye, ikabidi apige yowe kuita jina lake.
“Aligeuka kwa hasira na kusema, ‘Kwa nini
unaniijia hivyo?’
“Nikasema sikuwa. lakini nilitaka picha.
Alisema anataka usiku mtulivu.”
Usiku wa jana, Msemaji wa Cisse alisema:
“Kulikuwa kuna vijana wanne, ambao walianza kuleta usumbufu kwenye mlango wa
kuingilia. Walikuwa wanaita kwa sauti ‘Cisse’.
“Aliingia
ndani kuangalia filamu na wakaenda kumuomba radhi. Hao vijana wamekuwa waongo
sana. Hakukuwa na tukio kubwa,
0 comments:
Post a Comment