MSHAMBULIAJI Loic Remy amesherehekea kuhamia kwake Chelsea kwa kufunga bao pekee la ushindi Ufaransa ikiilaza Hispania 1-0 katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa.
Mchezaji huyo wa zamani wa QPR alitokea benchi kwenda kufunga bao hilo pekee zikiwa zimesalia dakika 16 mchezo kumalizika, akimtungua vizuri kipa wa Manchester United, David de Gea kumpa raha kocha Didier Deschamps Uwanja wa Stade de France.
Hispania ilitawala mchezo, lakini ikashindwa tu kutikisa nyavu za wenyeji huku kipa Hugo Lloris akiwas kikwazo kikuu kwao.



.png)
0 comments:
Post a Comment