• HABARI MPYA

    Thursday, September 18, 2014

    MAN CITY YAFA DAKIKA YA MWISHO MUNICH

    BAO pekee la Jerome Boateng dakika ya 89, limeipa ushindi mwembamba wa nyumbani, Bayern Munich wa 1-0 katika mchezo wake wa kwanza makundi Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku huu.
    Man City ilizuia vizuri mashambulizi ya Bayern kwa dakika 89 Uwanja wa Allianz Arena kabla ya kuachia dakika za mwishoni. Kocha Pep Guardiola aliyekuwa mnyonge muda wote wa mchezo, alitimka kwa kasi kutoka kwenye benchi kumfuata Boateng kushangilia naye bao hilo.
    Kikosi cha Bayern kilikuwa: Neuer, Rafinha/Pizarro dk84, Boateng, Benatia/Dante dk84, Bernat, Alaba, Lahm, Alonso, Muller/Robben dk76, Gotze na Lewandowski
    Man City: Hart, Sagna, Demichelis, Kompany, Clichy, Fernandinho, Yaya Toure, Navas, Silva, Nasri (Milner 58), Dzeko/Aguero dk74.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN CITY YAFA DAKIKA YA MWISHO MUNICH Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top