TIMU ya Hispania imeiadhibu Saudi Arabia kwa kuichapa mabao 4-0 usiku huu katika mchezo wa Kundi H Fainali za Kombe la Dunia Uwanja wa Mercedes-Benz Stadium, Atlanta, Georgia nchini Marekani.
Kiungo mshambuliaji wa Barcelona, Lamine Yamal Nasraoui Ebana mwenye asili ya Morocco kupitia kwa baba yake, Mounir Nasraoui na Equatorial Guinea kupitia kwa mama yake, Sheila Ebana – alifungua shangwe za mabao kwa Hispania dakika ya 10.
Mshambuliaji wa Real Sociedad, Mikel Oyarzabal Ugarte akafunga mabao mawili dakika ya 21 na 24, kabla ya beki wa kati wa Al Hilal ya kwao, Saudi Arabia Hassan Mohammed Osama Al-Tambakti kujifunga dakika ya 49 kuhitimisha nderemo za mabao kwa Hispani.
Kwa matokeo hayo, Hispania wanafikisha pointi nne na kupanda kileleni, wakifuatiwa na Saudi Arabia yenye pointi moja baada ya timu hizo zote kucheza mechi mbili.
Uruguay na Cape Verde ambazo zitamenyana baadaye Saa 7:00 usiku Uwanja wa Hard Rock, Miami Gardens, Florida, Marekani zote pia zina pointi moja moja baada ya mechi zao kwanza walizomaliza kwa sare dhidi ya Hispania na Saudi Arabia.



.png)
0 comments:
Post a Comment