• HABARI MPYA

    Friday, January 23, 2009

    NYOTA ALIYEUZWA KAMA MTUMWA UMANGANI

    Mshambuliaji Emanuel Gabriel Mwakyusa ambaye klabu yake, Simba ilimuuza Fanja ya Oman bila ya yeye kujua lolote. Hata hivyo, Fanja ilitumia busara kumshawishi nyota huyo akubali kwenda kujiunga nayo kwa kufanya naye mazungumzo upya juu ya dau la kumlipa. Kwa hilo, Gabriel alikubali na sasa yuko nchini humo akiitumikia Fanja, klabu yenye historia ya kufanyiwa kazi na Watanzania wengi, wakiwemo Talib Hilal, Ahmad Amasha, Hilal Hemed, Inno Haule, Ramadhan Lenny na wengineo. Kila la heri Gabriel.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    4 comments:

    Godfrey said... January 23, 2009 at 11:42 AM

    mawana mi naona kama jamaa kaonewa vile laikini ndio maisha mwache jamaa akatafute maisha lakini walichokifanya uongozi si chakiungwana ni hayo tu niliyokua nayo kwa ajli ya mwanetu gabriel

    Godfrey said... January 23, 2009 at 12:11 PM

    Kiukweli Mmi naona viongozi wa soka wa tz ndio wanaoendelea kuzorotesha soka la bongo inavyoonesha gabriel hakuwa tayari kuondoka simba lakini walichokifanya wao kumshawishi kwa nguvu ili akalicheze soka la ughaibuni kwa manufaa ya viongozi wenyewe na kwa kile nachoweza kukiita ni tamaa za viongozi wetu,wabadilike bwanaaa.

    Unknown said... January 23, 2009 at 12:28 PM

    KUNA KILA SABABU YAKULIVALIA NJUGA SUALA HILI ILI LISIENDELEE KUOTA MIZIZI KWANI TUKIZIDI KUKAA KIMYA WACHEZAJI HAWATANUFAIKA NA HAWATAJUA NI WAPI HAKI YAO KWAKUIPATA NINACHOKIOMBA WAWE WAWAZI KAMA WALIVYOFANYA KWA HENRY JOSEPH MBONA WAMEKUWA WAWAZI,KUNANINI KIMEJIFICHA KWA MWAKYUSA? VIONGOZI WA VILABU BADILIKENI NA MJITAHIDI KWENDA NA WAKATI MTAFICHA LEO KESHO WENYEWE MTAUMBUANA!!!!!!!!!

    Unknown said... January 23, 2009 at 12:32 PM

    wahenga wanasema kila mficha maradhi ujue kifo............! basi hicho ndicho kitachotokea kwa viongozi hao wakumbuke hata alex ferguson wa man united alikuwa anchukua asilimia kadhaa kwa wachezaji kwa siri na hatimaye akumbuka baada ya van neestroy kumuumbua hivyo ndivyo navyotegemea kwa mwakyusa naye ipo siku atatulipulia tu bomu mi yangu macho nakutegemea mzee wa blog kuweza kutunyetisha habari zilizo za motomoto,pamoja.

    Item Reviewed: NYOTA ALIYEUZWA KAMA MTUMWA UMANGANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top