• HABARI MPYA

    Monday, September 08, 2014

    BLATTER ATHIBITISHA KUGOMBEA TENA URAIS FIFA KWA MARA YA TANO MWAKANI

    KIGOGO  wa soka duniani, Sepp Blatter amethibitisha atasimama kugombea urais wa FIFA kwa mara ya tano mwakani.
    Blatter amekuwa akitarajiwa sana kugombea tena licha ya mwaka 2011 kusema hii itakuwa awamu yake ya mwisho na sasa amethibitisha atafanya hivyo. 
    Inafuatia Rais wa UEFA, Michel Platini kutangaza mwezi uliopita kwamba hatagombea uongozi FIFA.

    Amebadili mawazo: Sepp Blatter amethibitisha atagombea kwa mara ya tano Urais wa FIFA mwakani
    Out the running: UEFA president Michel Platini will not challenge Blatter for the high-profile position
    Nje ya mbio: Rais wa UEFA, Michel Platini hatashindana na Blatter kuwania nafasi hiyo ya juu katika ulimwengu wa soka

    Blatter amesema ataitambulisha rasmi Kamati Kuu ya FIFA juu ya mipango yake katika kikao cha Septemba 25 na 26.
    Babu huyo mwenye umri wa miaka 78 amesema hayo katika mahojiano ya video ya Soccerex katika Mkutano mjini Manchester: "Nitaithibitishia Kamati Kuu. ni suala la heshima  kusema hivyo, kisha kwenye familia ya soka, ndiyo nitakuwa tayari. Nitakuwa mgombea. Unaona mpango haujakamilika. Na mpango wangu haujaisha,"amesema.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BLATTER ATHIBITISHA KUGOMBEA TENA URAIS FIFA KWA MARA YA TANO MWAKANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top