KIUNGO Aaron Ramsey sasa atapambana na muda ili kupona maumivu aliyoyapata jana akiichezea nchi wake, Wales aweze kuichezea klabu yake, Arsenal mwshoni mwa wiki.
The Gunners itamenyana na Manchester City Jumamosi katika mchezo wa Ligi Kuu ya England wakati mchezaji wake huyo tegemeo aliumia jana Wales ikishinda 2-1 dhidi ya Andorra.
Kocha Chris Coleman amesema taarifa zaidi juu ya maumivu ya mchezaji huyo inaweza kutolewa saa 24 baadaye, jambo ambalo linamfanya kocha wa Arsenal, Arsene Wenger aanze kuumiza kichwa.
0 comments:
Post a Comment