• HABARI MPYA

    Sunday, September 07, 2014

    MECHI YA YANGA SC NA WAMALAWI YAOTA MBAWA

    MCHEZO kati ya Yanga SC na Big Gullets ya Malawi uliokuwa ufanyike jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam umefutwa kutokana na wageni kuharibikiwa na gari wakiwa njiani kuja nchini.
    Mashabiki kadhaa wa wamefika Uwanja wa Taifa kwa ajili ya kushuhudia mchezo huo, lakini kwa bahati mbaya wakakuta hakuna hata dalili.
    Taarifa zinasema Waandaaji wa mechi hiyo, Chama cha Soka Dar es Salaam  (DRFA) walifanya jiithada za kupata timu mbadala ya kucheza na Yanga, lakini zikashindikana.
    DRFA walijaribu kufanya mazungumzo hadi na Gor Mahia ya Kenya iliyofungwa 3-0 na Simba SC jana, lakini pia imeshindikana.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MECHI YA YANGA SC NA WAMALAWI YAOTA MBAWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top