KLABU ya Big Bullets iliyotangazwa kucheza mechi ya kirafiki na Yanga SC leo Dar es Salaam, jioni ya leo imetoka sare ya bila kufungana na Epac Uwanja wa Kamuzu mjini Blantyre katika Ligi Kuu ya TNM.
The Bullets sasa inashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi hiyo kwa pointi zake 36 baada ya mechi 17, sawa na vinara Moyale Barracks ambao wanaongoza kwa wastani wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Katikati ya wiki, Yanga SC ilitangaza mchezo wa kirafiki na timu hiyo ya Malawi kwamba utafanyika leo na baadaye Chama cha Soka Dar es Salaam (DRFA) kikasema, timu hiyo iliharibikiwa gari ikiwa njiani kuja Tanzania.
Usanii gani huu? Big Bullets waliodaiwa kuharibikiwa gari wakiwa njiani kuja Dar es Salaam, wamecheza mechi leo Ligi ya Malawi na kutoka sare 0-0
0 comments:
Post a Comment