Mshambuliaji wa KRC Genk, Mtanzania Mbwana Samatta akifarijiwa na mchezaji mwenzake, baada ya kukosa penalti dakika ya 74 katika sare ya 3-3 na wenyeji, Kortrijk kwenye mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza A Ubelgiji jana Uwanja wa Guldensporen mjini Kortrijk. Mabao ya Kortrijk yamefungwa na Mkongo Ilombe Mboyo mawili dakika za 63 na 83 na Mfaransa Idir Ouali dakika ya 70, wakati ya Genk yalifungwa na nyota wa Ukraine, Ruslan Malinovskiy dakika ya 50, Mghana Joseph Aidoo dakika ya 68 na Mbelgiji Leandro Trossard dakika ya 85
0 comments:
Post a Comment