Wachezaji wa Manchester United wakirejea katikati kinyonge baada ya Wolves kusawazisha bao katika sare ya 1-1 kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Old Trafford leo. United walitangulia kwa bao la mchezaji wake mpya, kiungo Frederico Rodrigues Santos 'Fred' dakika ya 18 akimalizia pasi ya Mfaransa Paul Pogba, kabla ya Joao Moutinho kuisawazishia Wolverhampton dakika ya 53 akimalizia pasi ya mshambuliaji Mmexico, Raul Jimenez. Mchezo huo ulihudhuriwa na kocha wa zamani wa Mashetani Wekundu, Sir Alex Ferguson kwa mara ya kwanza tangu aripotiwe kuugua Mei mwaka huu PICHA ZAIDI GONGA HAPA
Watch: Lille midfielder Ethan Mbappe shown red card for ugly elbow
-
Ethan Mbappé was shown a red card in Lille's Champions League match against
Real Betis on Tuesday.
18 hours ago



.png)
0 comments:
Post a Comment