• HABARI MPYA

    Wednesday, September 10, 2014

    ITALIA YAANZA VYEMA MBIO ZA EURO 2016, YAIFUMUA NORWAY 2-0 BARAZANI KWAKE

    ITALIA imeanza vyema kampeni za kufuzu Euro 2016 baada ya kuichapa Norway mabao 2-0 kocha Antonio Conte akiendeleza wimbi la ushindi katika mwanzo wake kazini.
    Simon Zaza alifunga bao lake la kwanza timu ya taifa dakika ya 16 katika mchezo ambao pengo la mshambuliaji Mario Balotelli anayetumikia adhabu halikuonekana sana, kabla ya beki wa kati wa Juventus, Leonardo Bonucci alifunga bao la pili dakika ya 62.
    Kikosi cha Norway kilikuwa: Nyland, Forren, Nordtveit, Elabdellaoui, Flo, Nielsen/Elyounoussi dk50, Johansen, Skjelbred/Pedersen dk75, Jenssen/Tettey dk70, Daehli na King.
    Italy: Buffon, Ranocchia, Bonucci, Astori, Giaccherini, Florenzi/Poli dk87, De Rossi, De Sciglio, Darmian/Pasqual dk61, Immobile na Zaza/Destro dk83.

    Raha ya ushindi: Zaza akishangilia na wachezaji wenzake baada ya ushindi wa jana
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ITALIA YAANZA VYEMA MBIO ZA EURO 2016, YAIFUMUA NORWAY 2-0 BARAZANI KWAKE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top