WINGA Angel di Maria ametengeneza mabao matatu na kufunga moja, Argentina ikilipa kisasi cha Kombe la Dunia kwa kuifunga 4-2 Ujerumani usiku huu katika mchezo wa kirafiki mjini Dusseldorf, Ujerumani.
Mchezaji huyo ghali zaidi kuwahi kusajiliwa Manchester United na Uingereza nzima alipika mabao ya Sergio Aguero, Erik Lamela na Federico Fernandez kabla ya kufunga na lake mwenyewe siku 52 tangu bao la Mario Gotze katika muda wa nyongeza liipe Ujerumani ubingwa wa dunia nchini Brazil.



.png)
0 comments:
Post a Comment