• HABARI MPYA

    Saturday, September 06, 2014

    NEYMAR AING'ARISHA BRAZIL IKIWACHAPA 1-0 COLOMBIA, FALCAO ACHEMSHA

    NAHODHA wa Brazil, Neymar jana alimfanya kocha mpya wa timu hiyo, Carlos Dunga aanze maisha vizuri baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Colombia katika mchezo wa kirafiki Uwanja wa Sun Light mjini Miami.

    Neymar alifunga bao hilo pekee dakika ya 83 katika mchezo ambao mshambuliaji mpya wa Manchester United, Radamel Falcao alitokea benchi dakika ya 77 kwenda kuchukua nafasi ya James Rodriquez, lakini hakufurukuta. 

    Colombia ilimpoteza winga wake Juan Cudrado aliyetolewa kwa kadi nyekundu kipindi cha pili.
    Kikosi cha Brazil kilikuwa: Jefferson, Maicon/Elias dk45, Miranda, David Luiz/Marquinhos dk80, Filipe Luis, Ramires/Fernandinho dk45, Luiz Gustavo, Willian/Coutinho dk72, Tardelli/Robinho dk77, Oscar/Everton Ribeiro dk72 na Neymar. 
    Colombia: Ospina; Zuniga/Mejia dk72, Zapata, Valdes, Armero; Cuadrado, Ramirez/Arias dk45, Sanchez/Ramos dk85, Rodriguez/Falcao dk77, Martinez/Guarin dk64 na Gutierrez/Bacca dk64.
    Nahodha babu kubwa: Neymar akimtoka beki wa Colombia, Juan Zuniga jana mjini MiamiCameo: Striker Radamel Falcao made a brief fifteen minute cameo for Colombia against Brazil
    Radamel Falcao akipambana katikati ya mabeki wa Brazil jana
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NEYMAR AING'ARISHA BRAZIL IKIWACHAPA 1-0 COLOMBIA, FALCAO ACHEMSHA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top