• HABARI MPYA

    Wednesday, May 20, 2026

    SERENGETI BOYS YACHAPWA NA MALI MABAO 2-1 AFCON U17


    TANZANIA imepoteza mechi yake ya mwisho ya Kundi C Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17(AFCON U17) kwa kuchapwa mabao 2-1 na Mali usiku huu Pitch 8 ya Uwanja wa Mohammed VI Football Academy Jijini Sale Kaskazini Magharibi mwa Morocco.
    Mabao yote ya Mali ‘The Eagles’ yamefungwa na mshambuliaji Abdoulaye Touré dakika ya nne na 34, wakati bao pekee la Serengeti Boys limefungwa na beki Hassan Azizi Mkinda dakika ya 82. 
    Mchezo mwingine wa mwisho wa Kundi C, Msumbiji imeichapa Angola mabao 2-1  Pitch 11 ya Uwanja huo huo wa Mohammed VI Football Academy.
    Kwa matokeo hayo, Tanzania imeongoza Kundi C kwa pointi sita, ikifuatiwa na Mali iliyomaliza na pointi tano na zote zinafuzu Robo Fainali pamoja na Fainali za Kombe la Dunia za U17 zinazotarajiwa kufanyika nchini Qatar kuanzia Novemba 19 hadi Desemba 13 mwaka huu. 
    Msumbiji iliyomaliza na pointi nne nafasi ya tatu pamoja na kutlewa kwenye fainali za AFCON U17, lakini inakwenda mchujo wa kuwania tiketi ya ambazo zote Fainali za Kombe la Dunia za U17.
    Mchujo huo utahusisha timu nne zilizomaliza nafasi ya tatu kwenye makundi yote manne, A,B,C na D na washindi wa mechi hizo wataungana na timu nane zilizoshka nafasi mbili za juu kwenye makundi hayo kwenda Qatar.
    Ikumbukwe Tanzania inashiriki Fainali za U17 kwa mara ya tatu baada ya mwaka 2017 nchini Gabon na 2019 Mumbai, Tanzania ambako mara zote walitolewa katika hatua ya makundi.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SERENGETI BOYS YACHAPWA NA MALI MABAO 2-1 AFCON U17 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top