TANZANIA imejiweka kwenye nafasi nzuri ya kwenda Robo Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON U17) baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Angola jioni ya leo Pitch 3 ya Uwanja wa Mohammed VI Football Academy Jijini Sale Kaskazini Magharibi mwa Morocco.
Mabao ya Serengeti Boys leo yamefungwa na Razaki Juma Mbegelendi dakika ya 27, Hassani Kizinga dakika ya 52 na Sadam Hussein Hamisi dakika ya 66.
Kwa ushindi huo, Serengeti Boys inafikisha pointi sita katika mchezo wa pili kufuatia kuichapa Msumbiji mabao 3-0 katika mchezo wa kwanza wa kundi hilo juzi na kujihakikishian pia tiketi ya kushiriki Fainali za Kombe la Dunia za U17 zinazotarajiwa kufanyika nchini Qatar kuanzia Novemba 19 hadi Desemba 13 mwaka huu.
Tanzania inweza kujihakikishia tiketi ya Robo Fainali kama Mali itaifunga Msumbiji katika mchezo mwingine wa Kundi C baadaye leo Pitch 8 ya Uwanja wa huo huo wa Mohammed VI Football Academy Jijini Sale.
Ikumbukwe Tanzania inashiriki Fainali za U17 kwa mara ya tatu baada ya mwaka 2017 nchini Gabon na 2019 Mumbai, Tanzania ambako mara zote walitolewa katika hatua ya makundi.
Ikumbukwe Tanzania inashiriki Fainali za U17 kwa mara ya tatu baada ya mwaka 2017 nchini Gabon na 2019 Mumbai, Tanzania ambako mara zote walitolewa katika hatua ya makundi.
.jpg)


.png)
0 comments:
Post a Comment