• HABARI MPYA

    Thursday, May 14, 2026

    CHAMA APIGA MBILI SIMBA YAICHAPA MASHUJAA FC 3-0 PALE PALE KIGOMA


    VIGOGO, Simba SC wamefufua matumaini ya ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya wenyeji, Mashujaa FC jioni ya leo Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma.
    Kiungo mshambuliaji wa Kimataifa wa Zambia, Clatous Chotta Chama amefunga mabao mawili dakika ya sita na 70, huku bao la tatu likifungwa na mshambuliaji mzawa, Suleiman Abdallah Mwalimu dakika ya 90’+2.
    Kwa ushindi huo, Simba SC wanafikisha pointi 52, ingawa wanabaki nafasi ya pili wakizidiwa pointi mbili tu na mabingwa watetezi, Yanga SC baada ya timu zote kucheza mechi 23.
    Kwa upande wao Mashujaa FC baada ya kupoteza mchezo huo wanabaki na pointi zao 26 za mechi 23 sasa nafasi ya tisa kwenye ligi ya timu 16. 
    Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu.
    Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndiye atacheza Ligi Kuu msimu ujao. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: CHAMA APIGA MBILI SIMBA YAICHAPA MASHUJAA FC 3-0 PALE PALE KIGOMA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top