• HABARI MPYA

    Friday, May 22, 2026

    FEI NA NADO WAFUNGA AZAM FC YAICHAPA TANZANIA PRISONS 2-0 CHAMAZI


    TIMU ya Azam FC imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
    Mabao ya Azam FC yamefungwa na kiungo Feisal Salum Abdallah dakika ya 15 kwa penalti na winga Iddin Suleiman Ally ‘Nado’ dakika ya 62.
    Kwa ushindi huo, Azam FC inafikisha pointi 49, ingawa inabaki nafasi ya tatu nyuma ya mabingwa watetezi, Yanga SC wenye pointi 57 na Simba SC pointi 55 baada ya timu hizo zote kucheza mechi 24.
    Kwa upande wao Tanzania Prisons baada ya kupoteza mchezo huo wanabaki na pointi zao 17 nafasi ya 15 kwenye ligi ya timu 16 mbele ya KMC wanaoshika mkia kwa pointi zao tisa baada ya timu hizo pia kucheza mech 24.i 
    Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja moja kwa moja, wakati nyingine mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu.
    Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndiye atacheza Ligi Kuu msimu ujao.   

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: FEI NA NADO WAFUNGA AZAM FC YAICHAPA TANZANIA PRISONS 2-0 CHAMAZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top