TIMU ya Pamba Jiji FC imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji, KMC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam.
Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, mshambuliaji Mkenya, Mathew Tegisi Momanyi dakika ya 57 na kwa ushindi huo, Pamba Jiji Fc inafikisha pointi 33 na kusogea nafasi ya saba, wakati KMC inaendelea kushika mkia kwenye ligi ya timu 16 ikibaki na pointi zake tisa kufuatia timu hizo kucheza mechi 24 kila moja.
Ikumbukwe mwisho wa msimu mbili zitashuka Daraja moja kwa moja, wakati nyingine mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu.
Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndiye atacheza Ligi Kuu msimu ujao.



.png)
0 comments:
Post a Comment