WENYEJI, TRA United wamelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na JKT Tanzania katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha.
Mshambuliaji Mganda, Joseph Akandwanaho alianza kuifungia TRA United dakika ya 20, kabla ya beki wa kulia, Salum Khamis Salum ‘Gado kuisawazishia JKT Tanzania dakika 10 baadaye.
Kwa matokeo hayo, TRA United inafikisha pointi 34, ingawa inabaki nafasi ya sita ikiendelea kuzidiwa pointi mbili na JKT Tanzania inayoshika nafasi ya tano baada ya timu hizo zote kucheza mechi 23.



.png)
0 comments:
Post a Comment