// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); HAZARD NDIYE MWANASOKA BORA WA MWAKA CHELSEA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE HAZARD NDIYE MWANASOKA BORA WA MWAKA CHELSEA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Tuesday, May 13, 2014

    HAZARD NDIYE MWANASOKA BORA WA MWAKA CHELSEA

    MWANASOKA Bora wa Mwaka wa Chelsea ni Eden Hazard, aliyeshinda tuzo hiyo na kukabidhiwa jana.
    Kiungo guti wa Ubelgiji alikuwa na msimu mzuri chini ya kocha Jose Mourinho, akifunga mabao 14 na kumaliza kama mfungaji bora wa klabu.
    Hazard, aliyetua Stamford Bridge akitokea Lille mwaka 2012, pia msimu huh ameshinda tuzo ya Mwanasoka Bora Chipukizi wa PFA, aliyokabidhiwa mwezi uliopita baada ya kumaliza katika nafasi ya pili nyuma ya nyota wa Liverpool, Luis Suarez aliyeshinda.
    Nyota kweli: Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho akimkabidhi Eden Hazard tuzo ya Mwanasoka Bora wa Mwaka wa klabu hiyo

    Pamoja na mabao hayo aliyofunga, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 alitoa pasi za mabao saba kuisaidia The Blues kumaliza katika nafasi ya taut kwenye Ligi Kuu ya England na kufika Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa.
    Mchezaji huyo aliyeripotiwa kutakiwa na Paris Saint-Germain alikuwa akikandiwa na Mourinho wiki za karibuni, lakini Special One ameonyesha hana kinyongo naye kwa kumkabidhi Hazard tuzo hiyo.
    Cesar Azpilicueta ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Wachezaji wa Mwaka baada ya kushinda jura za wachezaji wenzake tang aanze kucheza kikosi cha kwanza Novemba.
    Mspanyola huyo aliyempokonya namnba Ashley Cole tang wakati huo amekuwa beki wa kushoto chaguo la kwanza.Players' choice: Defender Cesar Azpilicueta (centre) poses with his Players' Player of the Year award and former Chelsea goalkeeper Carlo Cudicini (left)
    Chaguo la wachezaji: Beki Cesar Azpilicueta (katikati) akiwa amepozi na tuzo yake kwa pamoja na kipa wa zamani wa Chelsea, Carlo Cudicini (kushoto)
    Servant: Former Chelsea defender Paulo Ferreira picks up the club's Special Recognition award from Lord Sebastian Coe
    Gwiji: Beki wa zamani wa Chelsea, Paulo Ferreira akipokea tuzo maalum ya kutambuliwa kwa mchango wake kutoka kwa Lord Sebastian Coe
    Big future: Youngster Lewis Baker won the club's Young Player of the Year and Goal of the Season awards
    Kifaa cha baadaye: Kinda Lewis Baker ameshinda tuzo ya Mwanasoka Bora chipukizi wa Mwaka 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: HAZARD NDIYE MWANASOKA BORA WA MWAKA CHELSEA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top