• HABARI MPYA

    Monday, January 28, 2013

    BABU WA SIMBA 'HATUMI MTOTO DUKANI' MWANZO MWISHO

    Tofauti na makocha wengi wa Kizungu wanaokuja nchini kufanya kazi, katika mechi huwaachia Wasaidizi wao wazalendo majukumu ya kuzungumza na wachezaji mchezo unapoendelea, kocha wa Simba, Mfaransa Patrick Liewig juzi katika mechi dhidi ya African Lyon alikuwa akipigizana nao mwenyewe kelele, hadi kuna wakati mwamuzi wa akiba alisimama kumuamuru aketi kidogo baada ya kusimama muda mrefu mfululizo akisema nao.

    Babu Liewig anasema nao

    Babu anasema nao wakati wasaidizi wake wanakula kipupwe kwenye sofa

    Hapa refa anakuja kumuambia akae 

    Hapa Julio aliinuka kumsaidia kusema nao

    Refa anamuacha Julio asimame, anamuambia Babu akakae

    Babu anauliza, mbona Julio humuambii akae, refa anamuambia huyu kasimama sasa hivi, we tangu maechi ianze bwana hadi sasa hivi mnaongoza 3-1 bado hujakaa tu

    Babu kakubali yaishe anakaa

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: BABU WA SIMBA 'HATUMI MTOTO DUKANI' MWANZO MWISHO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top