Mfungaji wa bao la Azam leo, Samih Hajji Nuhu akipongezwa na Mwaikimba |
Na Prince Akbar
AZAM FC
imeanza vibaya ziara yake ya Kenya, baada ya kufungwa mabao 2-1 kwa tabu na
wenyeji AFC Leopard katika mchezo wa kirafiki uliofanyika kwenye Uwanja wa
Nyayo, Nairobi, jioni hii.
Mabao ya
washindi katika mchezo huo, yalifungwa na Paul Were na Mike Barasa, wakati la
Azam lilifungwa na Sammih Hajji Nuhu kwa penalti.
Hata hivyo,
Azam itabidi wajilaumu wenyewe kupoteza mchezo huo, kwani walipoteza penalti mbili
kupitia kwa Joackins Atudo na Khamis Mcha ‘Vialli’.
Pamoja na
kufungwa, Azam ilionyesha soka maridadi jioni ya leo mjini hapa kiasi cha kuwavutia
mashabiki wa Kenya, waliojikuta wakiishangilia baada ya kuzimikia soka yao.
Katika mchezo
huo, kikosi cha Azam FC kilikuwa; Mwadini Ally, Himid Mao, Samir Hajji Nuhu,
Luckson Kakolaki, Joackins Atudo, Abdulhalim Humud/Ibrahim Mwaipopo, Jabir
Aiziz/Humphrey Mieno, Salum Abubakar/Kipre Balou, Gaudence Mwaikimba/Brian Umony,
Khamis Mcha na Uhuru Suleiman/Abdi Kassim ‘Babbi’.
AFC Leopards: Martin Musalia, Edwin Wafula, Antony Kimani, Eric Masika, Noah Abich, Martin Imbalambala, Patillah Omoto, Bernard Mangoli, Victor Ochieng, Mike Baraza, Paul Were.
AFC Leopards: Martin Musalia, Edwin Wafula, Antony Kimani, Eric Masika, Noah Abich, Martin Imbalambala, Patillah Omoto, Bernard Mangoli, Victor Ochieng, Mike Baraza, Paul Were.