Na Baby Akwitende, Dar es Salaam
MASHINDANO ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati maarufu Kombe
la Kagame yamepangwa kufanyika kuanzia Agosti 9 hadi 23 mwaka huu jijini Kigali
nchini Rwanda.
Tanzania Bara itawakilishwa na Yanga katika mashindano hayo
yanayoandaliwa na Shirikisho la Soka Afrika Mashariki na Kati ( CECAFA).
Akizungumza na BIN ZUBEIRY jana , Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholas
Musonye, alisema timu zote wanachama wa shirikisho hilo zinatarajiwa kushiriki.
![]() |
| Kikosi cha Yanga SC |
Musonye alisema kuwa bado sekretarieti haijateua timu mwalikwa
katika mashindano hayo kutokana na mabadiliko ya kalenda ya michuano hiyo
ambayo hufanyika kila mwaka kati ya mwezi Mei na Juni.
"Ratiba kamili ya mashindano hayo itatolewa baadaye",
alisema Musonye.
Mlezi wa CECAFA na Rais wa Rwanda, Paul Kagame, ameshathibitisha
kutoa zawadiambayo ni Dola za Marekani 60,000 ambazo alianza kutoa tangu mwaka
2002.
Wadhamini wengine waliothibitisha kudhamini mashindano ya mwaka
huu ni kituo cha televisheni cha Super Sport.
Bingwa mtetezi wa mashindano hayo ni Atraco ya Burundi na mfungaji
bora wa michuano hiyo alikuwa ni Amissi Tambwe, anayeichezea Simba akitokea kwa
mabingwa hao.



.png)
0 comments:
Post a Comment