UWEZEKANO wa mabondia Floyd Mayweather Jnr na Manny Pacquiao kukutana ulingoni umezidi kuwa mdogo, baada ya Mfilipino kuongeza Mkataba na promota Top Rank.
Pacquiao amejifunga na Bob Arum hadi mwishoni mwa mwaka 2016, wakati ambao atakuwa anatimiza miaka 38 na wazi atakuwa anafikiria kustaafu.
Bingwa huyo wa maharaja name ya uzito tofauti duniani mapambano yake yanaonyeshwa na Televisheni ya HBO nchini Marekani, wakati Mayweather ana Mkataba na wapinzani, Televisheni ya Showtime, manna yake bambino baina ya wawili vigumu kuokea.
![]() |
| Vigumu sana; Manny Pacquiao sasa atapigana kwa mara ya tano na Juan Manuel Marquez baada ya kuongeza Mkataba na Top Rank, maana yake inaondoa uwezekano wa kupigana na Floyd Mayweather Jnr |
Mambo ulinglni: Mkataba mpya wa Pacquiao unazidi kuondoa uwezekano wa pambano lake na Floyd Mayweather
Mayweather amebakiza mapambano matatu kwenye Mkataba huo, utakaomalizika Septemba mwaka 2015.
Pamoja na hayo, Arum anahitaji cola za Kimarekani 300 ili bambino hilo liendelee kuwepo.
"Tunataka kupigana neya na tuko tayari kujadiliana kwa namna yoyote,"alisema. "Kuna njia mvili za kufanya hapa. Moja ni kulifanya pambano hili na Mayweather liwe la pamoja kati ya HBO na Showtime, kama walivyofanya kwa Lewis na Tyson, kama ninavyofahamu, Mayweather atakuwa ndani ya Mkataba na Showtime hadi mwaka 2015. Kampuni hizo zinaweza kuungana na kufanya kazi pamoja,".
"Au, namna nyingine ni, ikiwa Floyd anataka, apigane na Manny mwaka 2016, anaweza kurudi HBO na tunaweza kufanya kazi hapo,".
Mkongwe: Pacquiao sasa ameongeza Mkataba na Top Rank hadj mwaka 2016 atakapotimiza miaka 38
Utata wa bambino hilo unatokana na kuvunjika kwa uhusiano baina ya Arum na Mtendaji Mkuu wa Golden Boy, Richard Schaefer.
Mayweather alifanya kazi na Golden Boy kuanzia mwaka 2007 na bondia huyo mwenye umri wa miaka 37 atarejea ulingoni Septemba 13, baada ya kumtwanga Marcos Maidana mjini Las Vegas mapema mwezi huu.
Pacquiao, anaweza kuzipiga na Juan Manuel Marquez kwa mara ya tano mjini Macau, Novemba.



.png)
0 comments:
Post a Comment