// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); U15 YA TANZANIA YAWASILI GABORONE KUWANIA TIKETI YA FAINALI ZA AFRIKA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE U15 YA TANZANIA YAWASILI GABORONE KUWANIA TIKETI YA FAINALI ZA AFRIKA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Tuesday, May 20, 2014

    U15 YA TANZANIA YAWASILI GABORONE KUWANIA TIKETI YA FAINALI ZA AFRIKA

    Na Boniface Wambura, Dar es Salaam
    TIMU ya Tanzania ya umri chini ya miaka 15 imewasili salama jijini Gaborone, Botswana kwa ajili ya michezo ya Afrika ambapo itacheza mechi yake ya kwanza Mei 22 mwaka huu dhidi ya Mali.
    Kikosi hicho cha wachezaji 16 chini ya Kocha Abel Mtweve kimetua jijini Gaborone jana (Mei 19 mwaka huu) jioni kwa ndege ya South African Airways. Michezo hiyo itamalizika Mei 30 mwaka huu.

    Rais wa TFF, Jamal Malinzi (kulia) katikati amehakikisha U15 inashiriki mashindano
    Wachezaji waliopo kwenye kikosi cha Tanzania ni Adam Shayo, Amani Ally, Amos Manguli, Amri Nyuki, Amede Amani, Baraka Rashid, David Uromi, Goodlove Mdumule, Hance Msonga, Kelvin Kamalamo, Makalius Amrin, Nasson Chanuka, Paulo Ngowi, Petro Shaban, Rajab Mohamed na Thomas Chindeka.
    Nchi nyingine zinazoshiriki michezo hiyo kwa upande wa mpira wa miguu ni Afrika Kusini, Botswana, Nigeria, Mali na Swaziland.
    Gabon na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) ambazo nazo zilikuwa zishiriki kwenye michezo hiyo katika dakika za mwisho.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: U15 YA TANZANIA YAWASILI GABORONE KUWANIA TIKETI YA FAINALI ZA AFRIKA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top