KOCHA Louis van Gaal atakuwa analipwa mshahara wa Pauni Milioni 6 kwa mwaka na atapewa Pauni Milioni 200 kwa ajili ya kufanya usajili wa maana Manchester United.
Kocha huyo Mholanzi aliyeteuliwa kuchukua nafasi ya David Moyes, amesaini Mkataba wa miaka mitatu na kutangazwa rasmi mchana wa jana na atakuwa anasaidiwa na Ryan Giggs.
Klabu bado inataka kujumuisha watu watatu wa Class of 92 katika bench la Ufundi, Phil Neville, Nicky Butt na Paul Scholes -lakini bado hakuna uamuzi uliotolewa hadj sasa.
Van Gaal ataanza kazi rasmi baada ya Fainali za Kombe la Dunia mwezi ujao nchini Brazil ambako ataiongoza Uholanzi kwa mara ya mwisho.
Van Gaal anataka kuwasajili mabeki Wajerumani Mats Hummels na Holger Badstuber, viungo Toni Kroos na Arjen Robben na mshambuliaji Mario Mandzukic kuimarisha Man United ya kushindani mataji msimu ujao.

Kocha mpya: Louis van Gaal atapewa Pauni Milioni 200 za kufanyia usajili Manchester United
WANAOTAKIWA NA VAN GAAL...
KEVIN STROOTMAN
Roma Pauni Milioni 25, miaka 24
2013-14 mechi: 28 mabao: 6
Anatumia mguu wa kushoto, mtaalamu, lakini hana kasi. Anasumbuliwa na maumivu goto na hataweza kuingia uwanjani hadi Oktoba.
2013-14 mechi: 28 mabao: 6
Anatumia mguu wa kushoto, mtaalamu, lakini hana kasi. Anasumbuliwa na maumivu goto na hataweza kuingia uwanjani hadi Oktoba.
CESC FABREGAS
Barcelona Pauni Milioni 45, miaka 27
2013-14 Mechi: 55 Mabao: 13
Anauzwa. United inaweza kujaribu bahati yake.
2013-14 Mechi: 55 Mabao: 13
Anauzwa. United inaweza kujaribu bahati yake.
TONI KROOS
Bayern Munich Pauni Milioni 18, miaka 24
2013-14 Mechi: 51 Mabao: 4
Alikubali kujiunga na timu chini ya David Moyes. Van Gaal bado analitamani zao hilo la akademi ya Munich.
2013-14 Mechi: 51 Mabao: 4
Alikubali kujiunga na timu chini ya David Moyes. Van Gaal bado analitamani zao hilo la akademi ya Munich.
MATS HUMMELS
Borussia Dortmund Pauni Milioni 20, miaka 25
2013-14 Mechi: 28 Mabao: 2
Hayuko fiti sana lakini ni beki la kazi. Dortmund inaweza kumuuza
2013-14 Mechi: 28 Mabao: 2
Hayuko fiti sana lakini ni beki la kazi. Dortmund inaweza kumuuza
HOLGER BADSTUBER
Bayern Munich Pauni Milioni 15, miaka 25
2013-14 Hajacheza mechi hata moja, lakini mbele ya van Gaal huyo ndiye beki bora zaidi anayetumia mguu wa kuhsoto ndani ya Ujerumani.
2013-14 Hajacheza mechi hata moja, lakini mbele ya van Gaal huyo ndiye beki bora zaidi anayetumia mguu wa kuhsoto ndani ya Ujerumani.
LUKE SHAW
Southampton Pauni Milioni 27, miaka 18
2013-14 Mechi : 36 Hajafunga bao
Mchezaji huyo wa kimataifa wa England anaweza kujiunga na United mara sakata la ada ya uhamisho wake litakapomalizwa.
2013-14 Mechi : 36 Hajafunga bao
Mchezaji huyo wa kimataifa wa England anaweza kujiunga na United mara sakata la ada ya uhamisho wake litakapomalizwa.
SEBASTIAN JUNG
Eintracht Frankfurt Pauni Milioni 7, miaka 23
2013-14 Mechi: 36 Bao: 1
Beki wa kulia wa pili bora Ujerumani baada ya Philipp Lahm, ambaye Arsenal pia wanamtaka.
2013-14 Mechi: 36 Bao: 1
Beki wa kulia wa pili bora Ujerumani baada ya Philipp Lahm, ambaye Arsenal pia wanamtaka.
(Imeandaliwa na Simon Jones)
Winga teleza: Nyota wa Bayern Munich, Arjen Robben naye anatakiwa kocha van Gaal, ambaye pia ni kocha wake Uholanzi
0 comments:
Post a Comment