Mshambuliaji wa Simba SC, Emmanuel Okwi (kulia) akijivuta kupiga mpira dhidi ya beki wa Ndanda FC, William Lucian 'Gallas' katika mchgezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Simba ilishinda 1-0
Emmanuel Okwi (kulia) akikimbia na mpira dhidi ya beki wa Ndanda FC, Hemed Khoja
Winga wa Simba, Shiza Kichuya (kulia) akitafuta maarifa ya kumpita Jacob Massawe wa Ndanda
Nahodha wa Simba SC, John Bocco akiutuliza mpira mbele ya Ayoub Masoud wa Ndanda FC
Kiungo mshambuliaji wa Ndanda FC, Mrisho Ngassa akimiliki mpira katikati ya wachezaji wa Simba, Jonas Mkude (kushoto) na Erasto Nyoni (kulia)
Kiungo Mghana wa Simba SC, James Kotei akijaribu kumlamba chenga Omar Mponda wa Ndanda
Beki Mghana wa Simba, Asante Kwasi akimtoka Jacob Massawe wa Ndanda FC
Beki wa Ndanda FC, Ayoub Masoud akiteleza chini kuondosha mpira miguuni mwa Shomary Kapombe
Mmiliki mtarajiwa wa Simba SC, Mohammed Dewji (kushoto) akizungumza jambo na jamaa
Wachezaji wa akiba wa Simba, viungo Said Ndemla (kulia) na Muzamil Yassin (kushoto) wakifuatilia mchezo kwa makini
Emmanuel Okwi (kulia) akikimbia na mpira dhidi ya beki wa Ndanda FC, Hemed Khoja
0 comments:
Post a Comment