Mshambuliaji wa Barcelona, Luis Suarez (kushoto) akiwekeana mkwara na Sergio Ramos wa Real Madrid (kulia) wakati wa mechi ya La Liga baina ya mahasimu hao wa Hispania, maarufu kama El Clasico timu hizo zikitoa sare ya 2-2 usiku wa Jumapili. Mabao ya Barca iliyomaliza pungufu baada ya Sergi Roberto kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 45 na ushei yalifungwa na Luis Suarez dakika ya 10 na Lionel Messi dakika ya 52, wakati ya Real yalifungwa na Cristiano Ronaldo dakika ya14 na Gareth Bale dakika ya 72. Ronaldo alitolewa anachechemea na nafasi yake kuchukuliwa na Marco Asensio dakika ya 46 baada ya kuumia enka PICHA ZAIDI GONGA HAPA
'Stupid rumours' need to stop - Pochettino
-
Chelsea manager Mauricio Pochettino says the "stupid rumours’ about his
future need to end but admitted that he does not know if he and his staff
will be a...
25 minutes ago
0 comments:
Post a Comment