NYOTA wa filamu za kibabe, Sylvester Stallone 'Rambo' amepata msiba, baada ya mwanawe wa kiume, Sage kukutwa amekufa leo.
Taarifa za awali zinasema, kijana wake huyo mwenye umri wa miaka 36, alikutwa amekufa katika mjengo mmoja Los Angles na inasadikiwa 'aliji overdose' na maofisa wa Polisi wanachunguza kama kifo chake kilitokana na ajali au mauaji, kwa mujibu wa TMZ.
MSIBA: Huyu ndiye mtoto wa Sylvester Stallone 'Rambo', Sage aliyekutwa amekufa mchana wa leo Los Angeles baada ya kuji overdose dawa za kulevya. Alikuwa ana umri wa miaka 36 na picha hii alipigwa mwaka 2006 huko Hollywood
POLISI KATIKA ENEO LA TUKIO BAADA YA KUCHUKUA MWILI WA MAREHEMU
TABASAMU KWENYE ZULIA JEKUNDU: Sage alipigwa picha mwaka 1996 huko Hollywood katika uzinduzi wa Daylight akiwa na baba yake, Sylvester na mkewe Jennifer Flavin
ALIIGIZA NA BABA YAKE: Sage alishiriki na baba yake mwaka 1990 katika movie la Rocky V, akicheza kama mtoto wa Rocky (Rambo) Robert Balboa.
HII JANA TU: Stallone alipigwa picha na Arnold Schwarzenegger katika Comic Con ya filamu huko San Diego
IMETAFSIRIWA KUTOKA; http://www.dailymail.co.uk


.png)
0 comments:
Post a Comment