• HABARI MPYA

    Saturday, July 14, 2012

    ATLETICO WAIFUNDISHA SOKA YANGA

    Atletico wakishangilia bao la pili
    MABAO mawili ya Olivier Ndikumana katika dakika ya 81 na 90+3, jioni hii yameipa Atletico FC ushindi wa 2-0 dhidi ya mabingwa watetezi, Yanga katika mechi ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
    Yanga leo ilicheza ovyo na ilizidiwa katika kila idara- angalau baada ya kufungwa bao la kwanza walijaribu kushambulia kwa mipira ya pembeni, lakini walipopigwa la pili katika dakika ya tatu ya muda wa nyongeza baada ya kutimu kwa dakika 90 za mchezo huo ‘walitepeta kabisa’.
    Katika mechi ya kwanza ya kundi hilo, APR ya Rwanda iliitandika 7-0 Waw Salam ya Sudan Kusini.
    Baada ya mechi hiyo, kocha wa Yanga, Tom Saintfiet alisema kwamba Atletico ni timu nzuri na  na walicheza vizuri, lakini timu yake haikuwa vizuri leo. Aidha, alisema alipokuja Yanga aliambiwa timu hiyo inacheza mpira wa kukimbiza, ambao yeye hakuutaka.
    "Nataka wacheze soka ya utulivu, lakini leo mambo hayakuwa mazuri, taratibu timu itaendelea kuimarika na bado nina matumaini ya kufanya vizuri,"alisema.
    Lakini kocha wa Atletico, Kaze Cedric aliiponda safu ya ulinzi ya Yanga, kwamba ilikuwa butu. "Niliiogopa Yanga, nilijua ina wachezaji wazuri, tulijua tutapata upinzani mkubwa, lakini nashukuru tumeshinda. Tulijua Yanga wana kasi, tukaanza kwa kuwatuliza,"alisema Kaze.
    Refa wa mechi ya leo, Dennis Batte wa Uganda

    Huyu kipa aliyedaka leo Atletico, anaitwa Kaseja kwa jina la utani, ila jina lake halisi ni Said Ndikumana


    Kampeni zinaendelea

    Yanga kama wamemwagiwa maji, kufungwa noma

    Mtakatifu Tom akimpa 'bravo' kocha wa Atletico, Kaze


    Yanga wapolee

    Muuwaji wa Yanga, Olivier Ndikumana alivaa jezi namba 7
    Hatari kwenye lango la Atletico
    Sekeseke langoni mwa Atletico


    Kizaa zaa langoni mwa Atletico


    Yanga wanapiga mishe mishe za bao, ila Kaseja wa Burundi anadaka


    Refa Batte anasemezana nao Yanga, washamdondoisha Kaseja chini katika mishe za kusaka bao



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ATLETICO WAIFUNDISHA SOKA YANGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top